Wednesday, August 28, 2013
Friday, July 12, 2013
MASOGANGE AMEKAMATWA
Thursday, June 27, 2013
Ally Mzich Akiwa na Dj Choka
Mmoja Kati ya Waasisi Wanaounda Kundi la Muziki wa Hip Hop (Mazich Reality) Mjini Dodoma.
Kushoto Ally Mzich akiwa Dj Choka, Katika Ma Dj Bora Nchini Tanzania na Afrika Yote
Kushoto Ally Mzich akiwa Dj Choka, Katika Ma Dj Bora Nchini Tanzania na Afrika Yote
ASKOFU THABO MAKGOBA AFANYA MAOMBI MAALUM KWA AJILI YA MANDELA
Askofu mkuu wa kanisa la kianglikana mjini Cape Town,
Afrika Kusini, Thabo Makgoba, amejitolea kufanya maombi kwa niaba ya
rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anaugua sana hospitalini.
Kasisi huyo anamuombea Mandela aweze kupata nafuu na amewataka wananchi kumshukuru kwa yote aliyowafanyia.Jamaa za Nelson Mandela wamekutana nyumbani kwake huko Kunu, huku hali yake ya afya ikizidi kudorora hospitalini, Pretoria.
Afya ya Bwana Mandela ilikuwa mbaya zaidi Jumapili.
Maombi hayo yalitolewa baada ya Askofuu huyo kumtembelea Mandela hospitalini ambako kiongozi huiyo wa zamani amekuwa akilazwa kwa wiki mbili na nusu zilizopita baada ya kuugua mapafu.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa wajukuu wa rais huyo wa zamani wa Afrika kusini wanakutana nyumbani kwake kijijini katika mkoa wa Eastern Cape province, ambako viongozi wa kitamaduni wamealikwa.
Halikopta ya jeshi kadhalika zilionekana zikipaa karibu nyumbani kwa mandela. Afisi ya Rais jacob Zuma ilitangaza jumapili kuwa hali ya mzee Mandela ya afya ilikuwa mbaya sana.
UJIO WA RAIS BARAKA OBOMA NCHINI TANZANIA
Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya
nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya
Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai.
Katika
ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka
katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za
Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo
ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji
wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi
wa Kiafrika.
Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na
jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa
kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
Wednesday, June 26, 2013
Hali ya wasiwasi kuhusu afya ya Mandela
Wananchi wa Afrika Kusini wamekuwa na
wasiwasi baada ya rais wa nchi hiyo Jacob Zuma kutangaza kuwa hali ya
afya ya rais mstaafu Nelson Mandela sio nzuri sana.
Asubuhi waliamkia kwenda kazini wasijue taarifa watakazopokea baada ya rais Zuma kutoa taarifa hiyo.Taarifa zinazohusiana
Afisaa mmoja mkuu alisema kuwa raia wa Afrika Kusini wasiwe na matumaini kupita kiasi.
Mandela ambaye alikuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, akiwa na umri wa miaka 94,alipelekwa hospitalini mapema mwezi huu, ikiwa ni mara ya tatu kwake kulazwa hospitalini akiugua ugonjwa wa mapafu mwaka huu.
Rais Jacob Zuma alisema Jumapili kuwa alimzuru Mandela Hospitalini na kuzungumza na mkewe kuhusu hali ya rais mstaafu.
Madaktari wanaomtibu Mzee Nelson Mandela wamesema hali yake imekuwa sio nzuri kwa saa ishirini na nne zilizopita na sasa ni mahututi.
Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika Kusini.
Taarifa hiyo imesema bado Mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini Pretoria kwa siku ya kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyosababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais Jacob Zuma amemtembelea Mzee Mandela na pia kuzungumza na jopo la matabibu wanaomtibu.
Baadaye bwana Zuma alirejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea Mzee Mandela apate nafuu.
Tuesday, June 25, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)